BREAKING NEWS

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo HABARI. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo HABARI. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 5 Septemba 2016

Majina mashuhuri zaidi ya watoto


 Mtoto
TJina Noah limeingia kwenye orodha ya majina 10 mashuhuri zaidi kwa kupewa watoto wavulana kwa mara ya kwanza, huku Amelia likisalia kuwa jina ambalo wazazi wengi wanawapa watoto wasichana England na Wales, taasisi ya taifa ya Takwimu Uingereza imeonesha.
Jina Oliver ndio linaloongoza upande wa wavulana, likishikilia nafasi ya kwanza tangu 2013 nalo Amelia likiwa juu kwa wasichana tangu 2011. Watoto walioitwa Oliver mwaka 2015 ni 6,941 na Amelia 5,158.
Maafisa wa ONS waliorodhesha majina kando kwa mujibu wa jinsi jina liliandikwa.
Iwapo majina yanayotamwa kwa njia sawa yangewekwa pamoja, basi orodha hiyo huenda ingelikuwa tofauti kidogo.
Mfano ni jina Muhammad ambalo linashikilia nafasi ya 12 likiwa na watoto 3,730.
Kuna wazazi walioandika jina hilo kama Mohammed (2,332) na wengine kama Mohammad (976). Iwapo majina hayo yangejumlishwa, basi jina hilo lingelikuwa katika 10 bora.
Yalikuwepo majina ya kushangaza. Kwa mfano watoto wavulana 17 na wasichana 15 walipewa jina Baby.
Majuzi, utafiti ulionesha karibu sehemu moja kati ya tano ya wazazi Uingereza wanajutia majina waliyowapa watoto wao.
Image copyright Alamy
Image caption Rocky Balboa na Apollo Creed
Wavulana 35 walipewa jina Rocky, na 21 wakapewa Apollo, labda kutokana na wahusika wakuu wa filamu ya ndondi Rocky Balboa na Apollo Creed.
Wavulana 15 walipewa jina Blue na wengine 14 wakaitwa Ocean. Na kunao 18 walipewa jina Blu.
Kuna jumla ya wavulana 36 ambao watahitajika kujifunza kuandika na kutamka jina lao, Tymoteusz.
Image copyright PA
Image caption Wasichana watano wameitwa Kaleesi
Upande wa wasichana 280 walipewa jina Arya, mmoja wa wahusika wakuu filamu ya Game of Thrones, na wengine 562 wakaitwa Aria, 33 Ariah, 17 Aaria na sita Aariah, jina ambalo huenda ni moja ila likaandikwa tofauti.
Jina Kaleesi, pia kutoka kwa filamu hiyo, lilipewa wasichana watano.
Jina Princess lilipewa wasichana 72, ikikaribia wavulana 77 walioitwa Prince.
Image copyright Alamy
Image caption Perhaps boys called Maverick will grow up to become a Top Gun in whatever they do
Takwimu hizo zinaonesha jina Oliver ndilo maarufu zaidi kwa wavulana maeneo yoteb ya Englandisipokuwa London na West Midlands, ambapo jina Muhammad linaongoza.
Jina Muhammad lilipita Oliver eneo la West Midlands mwaka 2014.

Majina mashuhuri zaidi 2015
Image caption Jina la marehemu Oliver Reed linasalia kuwa maarufu zaidi kupewa wavulana
  • Oliver 6,941
  • Jack 5,371
  • Harry 5,308
  • George 4,869
  • Jacob 4,850
  • Charlie 4,831
  • Noah 4,148
  • William 4,083
  • Thomas 4,075
  • Oscar 4,066

Majina maarufu kwa wasichana 2015
Image copyright EPA
Image caption Amelia Boynton Robinson, mwanaharakati mtetezi wa haki za raia Marekani, alifariki mwaka jana akiwa na umri wa miaka 104
  • Amelia 5,158
  • Olivia 4,853
  • Emily 3,893
  • Isla 3,474
  • Ava 3,414
  • Ella 3,028
  • Jessica 2,937
  • Isabella 2,876
  • Mia 2,842
  • Poppy 2,816

Image copyright Reuters
Image caption Wasichana kadha pia wamepewa jina la mwanamuziki Rihanna
Wasichana 72 walipewa jina Adele, 39 wakaitwa Paloma, kutokana na mwanamuziki Paloma Faith.
Kulikuwa na wasichana 35 walioitwa Rihanna, na tisa Rhianna.
Majina 50 mashuhuri zaidi ya wavulana na wasichana England na Wales mwaka 2015
Wavulana Wasichana






Nambari Jina Watoto Nambari Jina Watoto






1 OLIVER 6941 1 AMELIA 5158
2 JACK 5371 2 OLIVIA 4853
3 HARRY 5308 3 EMILY 3893
4 GEORGE 4869 4 ISLA 3474
5 JACOB 4850 5 AVA 3414
6 CHARLIE 4831 6 ELLA 3028
7 NOAH 4148 7 JESSICA 2937
8 WILLIAM 4083 8 ISABELLA 2876
9 THOMAS 4075 9 MIA 2842
10 OSCAR 4066 10 POPPY 2816
11 JAMES 3912 11 SOPHIE 2779
12 MUHAMMAD 3730 12 SOPHIA 2744
13 HENRY 3581 13 LILY 2711
14 ALFIE 3540 14 GRACE 2658
15 LEO 3468 15 EVIE 2529
16 JOSHUA 3394 16 SCARLETT 2285
17 FREDDIE 3219 17 RUBY 2215
18 ETHAN 2940 18 CHLOE 2158
19 ARCHIE 2912 19 ISABELLE 2119
20 ISAAC 2829 20 DAISY 2113
21 JOSEPH 2786 21 FREYA 2090
22 ALEXANDER 2759 22 PHOEBE 2081
23 SAMUEL 2705 23 FLORENCE 2053
24 DANIEL 2622 24 ALICE 2006
25 LOGAN 2610 25 CHARLOTTE 1951
26 EDWARD 2593 26 SIENNA 1941
27 LUCAS 2448 27 MATILDA 1774
28 MAX 2407 28 EVELYN 1770
29 MOHAMMED 2332 29 EVA 1753
30 BENJAMIN 2328 30 MILLIE 1673
31 MASON 2263 31 SOFIA 1640
32 HARRISON 2241 32 LUCY 1525
33 THEO 2103 33 ELSIE 1513
34 JAKE 2013 34 IMOGEN 1478
35 SEBASTIAN 1988 35 LAYLA 1428
36 FINLEY 1978 36 ROSIE 1403
37 ARTHUR 1966 37 MAYA 1354
38 ADAM 1903 38 ESME 1340
38 DYLAN 1903 39 ELIZABETH 1338
40 RILEY 1728 40 LOLA 1322
41 ZACHARY 1644 41 WILLOW 1308
42 TEDDY 1430 42 IVY 1275
43 DAVID 1394 43 ERIN 1249
44 TOBY 1363 44 HOLLY 1248
45 THEODORE 1302 45 EMILIA 1243
46 ELIJAH 1294 46 MOLLY 1215
47 MATTHEW 1279 47 ELLIE 1185
48 JENSON 1223 48 JASMINE 1182
49 JAYDEN 1219 49 ELIZA 1171
50 HARVEY 1190 50 LILLY 1146

Kiir akubali wanajeshi wa UN watumwe Juba, Sudan Kusini

Wanajeshi wa UN

Wanajeshi hao wapya watatoka Ethiopia, Kenya, Rwanda, Sudan na Uganda
Rais wa Sudan Kusini hatimaye amekubali kikosi cha ziada cha wanajeshi wa kulinda amani kitumwe nchini humo.
Rais Salva Kiir alichukua hatua hiyo baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Bw Kiir alikuwa awali amekataa kutumwa kwa wanajeshi hao 4,000 kutoka mataifa ya kanda, akisema huo ni ukiukaji wa uhuru wa Sudan Kusini.
UN iliidhinisha kutumwa kwa wanajeshi hao baada ya kuzuka upya kwa vita baina ya wanajeshi waaminifu kwa Bw Kiir na aliyekuwa makamu wake wa rais Dkt Riek Machar mwezi Julai mjini Juba.
Kikosi hicho cha ziada kitakuwa na mamlaka zaidi kushinda kikosi cha sasa cha wanajeshi 13,000 ambacho kimekuwa kikihudumu nchini humo

Jumanne, 26 Julai 2016

Riek Machar ''apinduliwa'' Sudan Kusini


Image captionTaban Deng Gai
Maafisa wa serikali ya Sudan Kusini wameiambia BBC kwamba wanamtambua waziri wa madini Taban Deng Gai kuwa makamu wa kwanza wa rais akichukua mahala pake Riek Machar ambaye alitoroka mji mkuu wa Juba baada ya mapigano makali mapema mwezi huu.
Hatahivyo msemaji wa Machar amesema kuwa wameukataa uteuzi wa Bwana Deng.
Bwana Deng alikuwa mpatanishi mkuu wa Machar na hatua yake ya kuchukua wadhfa huo unaonyesha kuwa wametofautiana, hivyobasi kuweka mgawanyiko katika upinzani ambao unazidi kutatiza juhudi za kupata amani nchini Sudan Kusini ,kulingana na wachanganuzi.
Image copyrightREUTERS
Image captionWananchi wa Sudan Kusini wakiangalia runinga
Takriban watu 300 walifariki katika mapigano mapema mwezi huu katika mji mkuu wa Juba,kati ya vikosi vilivyo vitiifu kwa Machar na mpinzani wake rais Salva Kiiir

Nduguye Obama kumpigia kura Donald Trump


TrumpImage copyrightREUTERS
Image captionBw Malik amesema angependa sana kukutana na Bw Trump
Nduguye wa kambo wa Rais wa Marekani Barack Obama, Malik, ametangaza kwamba atampigia kura mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump.
Malik ameamua kutounga mkono chama cha Democratic chake Rais Obama ambacho mgombea wake ni Hillary Clinton.
Amesema anampenda sana Bw Trump kutokana na “uwazi wake” na kuongeza kwamba amesikitishwa sana na uongozi wa Rais Obama.
Ameambia BBC kwamba anaamini BwTrump, ni mtu mwenye huruma, mkweli na mwenye ushawishi.
"Akizungumza kwenye runinga anaonekana mtu anasemaye ukweli, kuhusiana na dunia kwamba imeharibika na hakuna usalama,” amesema Bw Malik.
Malik, 58, kwa muda mrefu alikuwa mfuasi wa chama cha Democratic lakini anasema utawala wa nduguye umemfanya kubadilika na kuanza kuunga mkono Bw Trump.
Akizungumza awali na gazeti la New York Post la Marekani, Malik alisema jambo lililomtamausha zaidi ni hatua ya mkuu wa shirika la ujasusi la Marekani FBI James Comey kupendekeza Bi Clinton asishtakiwe kutokana na hatua yake ya kutumia sava ya kibinafsi ya barua pepe akiwa waziri wa mambo ya nje.
Hajafurahia pia kwamba Bi Clinton na Rais Obama waliongoza vita vilivyopelekea kuuawa kwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi ambaye anasema ni mmoja wa marafiki zake wakuu.
Pia, hafurahishwi na hatua ya chama cha Democratic cha Marekani kuunga mkono ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
“Nampenda Donald Trump kwa sababu anazungumza kutoka moyoni. Ningependa kukutana naye,” anasema.
Baba yao Barack Obama Sr., aliondoka Kenya mwaka 1959 Malik alipokuwa na umri wa mwaka mmoja na akajiunga na chuo kikuu cha Hawaii, ambapo alikutana nan a baadaye akamuoa mamake Rais Obama, Stanley Ann Dunham.
Image copyrightAP
Malik Obama alikutana na Obama mara ya kwanza 1985.
Wawili hao hata hivyo wamekuwa wakigombana. Malik amekuwa akimshutumu nduguye akisema hajakuwa akimsaidia.
Malik aliwania ugavana Siaya katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2013 lakini akashindwa.
Amesema amejiandikisha kama mpira kura katika jimbo la Maryland na anapanga kupiga kura mwezi Novemba.
Bw Malik amesema hakuna uhasama mkubwa kati yake na Rais Obama lakini hamuamini sana. Amesema wakati Rais Obama alipokuwa akiomba kura alizungumza sana zake Kenya lakini alipoingia uongozini hajakuwa akiwasiliana nao sana.

Jumamosi, 16 Julai 2016

Wanajeshi waasi 104 wauawa Uturuki



Image copyrightGETTY
Naibu mkuu wa jeshi la Uturuki ametangaza kwa njia ya runinga kuwa jaribio la mapinduzi ya kijeshi limeshindwa.
Jenerali Umit Dundar alisema kuwa wapanga mapinduzi 104 wameuauwa. Pia amesema kuwa watu wengine 90 wakiwemo polisi na raia wameuawa.
Usiku kucha miji ya Ankara na Istanbul ilikumbwa na milio ya risasi na milipuko baada ya wanajeshi waasi kufanya mashambulizi wakitumia vifaru na helikopta.
Maafisa wanasema kuwa zaidi ya wanajeshi 1500 wamekamatwa huku wale wa vyeo vya juu wakiwemo majerali wakipokonywa nyadhifa zao.

Unyonyaji kidole unafaida kwa watoto- Utafiti


Image copyrightTHINKSTOCK
Image captionUnyonyaji kidole unafaida kwa watoto- Utafiti
Ripoti mpya inasema watoto wanaonyonya vidole au kung'ata kucha zao kwa meno huenda wasipate matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani.
Kwa mujibu wa waandishi katika jarida la Pediatrics, huo ni ni usafi dhanio,kwani yatokanayo na baadhi ya wadudu huimarisha mfumo wa kinga ya mwili.
Unyonyaji wa kidole gumba na ung’ataji wa kucha umeonekana kuzuia baadhi ya alergy.
Kati ya watu elfu moja wenye umri wa kati ya miaka mitano hadi thelathini na mbili,walifanyiwa uchunguzi kwa muda nchini New Zealand.
Lakini tabia hii ya unyonyaji vidole na ung’ataji kucha haisaidii watu wenye pumu au mtu anapopata homa kali.
Uchunguzi uliofanywa na kurekodiwa kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka mitano na kumi na moja na wengine waliofanyiwa vipimo ni wenye umri kati ya miaka kumi na tatu na thelathini na miwili.
Huku thuluthi moja ya watoto hao ni wanyonyaji wa vidole mara kwa mara au hung’ata kucha zao na katika vipimo walivyofanyiwa watoto hao wameonekana kuwa wana kiwango kidogo cha kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani.
Image copyrightTHINKSTOCK
Image captionLakini tabia hii ya unyonyaji vidole na ung’ataji kucha haisaidii watu wenye pumu au mtu anapopata homa kali.
Watoto wanaoweza kupata matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani (alergy) kutokana na vitu kama vumbi kutoka majumbani,manyoya ya paka au mbwa, lakini watoto wenye kunyonya vidole gumba na kung’ata kucha walikuwa ni chini ya theluthi moja kuliko watoto wenye tabia hii ya unyonywaji vidole.
Na tabia hii ya unyonyaji vidole au ung’ataji kucha inaonekana kuwa kinga mpaka wanapofikia umri wa utu uzima.
" kuwa na paka au mbwa majumbani,ndugu au jamaa wanaofanya kazi mashambani pia imeonekana kuwa ni sababu kubwa inayosababisha mazingira ya ukuaji wa magonjwa yanayosababishwa na
kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani

Mamia wapigwa picha wakiwa utupu Uingereza


Alfred GelderImage copyrightAFP
Image captionBarabara ya Alfred Gelder iligeuzwa kuwa bahari ya watu
Watu zaidi ya 3,000 walipigwa picha wakiwa utupu nchini Uingereza chini ya mradi wa kuadhimisha na kusherehekea utamaduni.
Mradi huo uliopewa jina Bahari ya Hull unatumiwa kusherehekea mji wa Hull kama Mji wa Utamaduni kwenye sherehe kuu mwaka ujao.
Baraza la Jiji la Hull lilisema mradi huo wa sanaa, ndio mkubwa zaidi wa aina yake kufanyika Uingereza.
Image copyrightAFP
Uliendeshwa na mpigapicha mashuhuri duniani Spencer Tunick na kushirikisha watu 3,200 kutoka nchi 20, ambao walipigwa picha katika maeneo mbalimbali maarufu mjini humo Jumamosi iliyopita.
WalioshirikiImage copyrightREUTERS
Image captionWatu wa kujitolea kutoka nchi 20 walishiriki
Picha hizo, ambazo zinasimamiwa na shirika la maonesho ya Sanaa la Ferens Art Gallery, zitawekwa kwenye maonesho wakati wa shughuli za Jiji la Utamaduni Uingereza mwaka 2017.
Maelfu ya watu walifika kabla ya jua kuchomoza na wakapakwa rangi ya samawati iliyokozwa kwa viwango vinne, kuashiria maji.

Walipigiwa picha maeneo mbalimbali yakiwemo Bustani ya Malkia, Guildhall na daraja la Scale Lane.
Shughuli yote ilidumu saa nne.
Image copyrightAP
Mmoja wa walioshiriki alikuwa Stephane Janssen, mwenye umri wa miaka 80 anayetoka Brussels.
Ameshiriki miradi ya upigaji picha wa watu wengi wakiwa utupu ya Tunick mara 20 awali.
TunickImage copyrightPA
Image captionBw Tunick (kushoto) akiwa na Janssen
“Ni maridadi sana, ni kupakwa rangi kidogo tu. Kila mtu ni sawa – hakuna tofauti ya rangi au jinsia – kila mtu ni sawa na yule mwingine akiwa utupu, na hilo ndilo napenda,” alisema.
Sarah Hossack, kutoka Hull, alisema alifurahia sana.
Image copyrightAFP
“Nilikuwa utupu tangu saa kumi alfajiri. Lakini nilifurahia sana. Shughuli hiyo ilituleta pamoja,” alisema.
Mradi huo wa Hull uliushinda ule wa Gateshead wa mwaka 2005 ambapo ni watu 1,700 waliojitokeza pamoja na ule wa Salford wa mwaka 2010 ambapo watu 1,000 walishiriki.
Image copyrightAFP
Kirsten Simister, afisa katika Ferens Art Gallery, alisema alishangazwa sana na idadi ya watu waliojitokeza Hull.
Tunick, ambaye makao yake ni New York, amefanya miradi mingine 90 kama huo wa Hull.
Amewahi kupigia watu wengi kwa pamoja picha katika Sydney Opera House, Place des Arts mjini Montreal, Mexico City na Munich nchini Ujerumani.

Bikizee wa miaka 94 arejea kazini Marekani


SoskinImage copyrightAP
Image captionBi Soskin (kati) alipokelewa kwa furaha kuu na wafanyakazi wenzake
Mama mmoja Mmarekani mwenye umri wa miaka 94 amerudi kazini kama askari waitwao Park Pangers wa kuhuduma katika mbuga na hifadhi za kitaifa nchini Marekani.
Bi Betty Reid Soskin, alikuwa ameacha kazi baada ya mkasa kumkumba ulimfanya.
Katika mkasa huo mwizi alimvamia nyumbani kwake tarehe 27 Juni, akamgonga ngumi kichwani na kumwibia simu, tarakilishi, vito vya thamani na hata medali yake aliyokuwa ametunukiwa na rais Obama.
Lakini anasema alitaka sana kurejelea maisha aliyoyazoea.
Bi Soskin, alikuwa mwelekezi katika hifadhi ya kihistoria iliyoko eneo la San Francisco Bay kwa muda wa miaka 10.
Kama anavyoonekana katika picha hizo za makaribisho ya wafanyikazi wenzake hapo hifadhi ya Rosie the Riveter World War Two Home Front National Historical Park ni vigumu kukadiria umri wakeread more.

Wafungwa 3 wauwa gerezani Thailand




Image copyrightEPA
Wafungwa watatu wameuawa wakati wa maandamano kwenye gereza moja lililo kusini mwa Thailand.
Karibu wafungwa 100 walishiriki katika ghasia hizo kwenye gereza moja lililo mkoa wa Pattani, ambazo zilidumu kwa muda wa saa sita.
Wafungwa hao kwanza walichoma majengo mawili ndani ya gereza hilo.
Wafungwa hao walikuwa wametangaza matakwa kadha ikiwemo kutembelewa zaidi na familia zao na pia kupewa fursa ya kutizama habari kwenye runinga.

SOMA ZAIDI HAPA