Maandamano yalianza Burundi Aprili mwaka jana
Mahakama ya rufaa nchini Burundi imewahukumu washtakiwa 21 vifungo vya maisha jela baada ya kuwapata na hatia ya kushiriki jaribio la mapinduzi mwaka jana.
Washtakiwa hao ni kati ya 28 waliokuwa wameshtakiwa kuhusiana na jaribio hilo la Mei mwaka jana ambalo halikufaulu.
Miongoni mwao ni watano ambao walikuwa wamepatikana bila hatia na mahakama ya kwanza.
Mahakama hiyo ya rufaa imeagiza wakamatwe.
Upande wa mashtaka ulikata rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa na mahakama ya chini ukisema hukumu hiyo haikuwa kali vya kutosha.
UN: Watu 474 wameuawa Burundi
Mataifa ya Kifaransa yavunja uhusiano wao na Burundi
Wale waliopatikana na hatia pia wametakiwa kulipa zaidi ya $3.5m (£2.4m) kama fidia kutokana na vifo na uharibifu wa mali uliotokea wakati wa jaribio hilo la kupindua serikali.
Baadhi ya majenerali kwenye jeshi na baadi ya maafisa wakuu katika idara ya polisi walijaribu kumpindua Rais Pierre Nkurunziza baada yake kuamua kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi wa leo unatazamwa kama ushindi wa serikali ambayo imekuwa ikijaribu kujenga uhusiano wa moja kwa moja baina ya jaribio hilo la mapinduzi na maandamano ya kupinga hatua ya Rais Nkurunziza kuwania kwa muhula wa tatu.
Maandamano hayo yalianza wiki mbili kabla ya mapinduzi.
BREAKING NEWS
-
Bonyeza hapa kuyaangalia moja kwa moja...
-
Image caption Magufuli: AirTanzania kupaa tena kufikia mwisho wa mwezi Septemba mwaka huu Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amet...
Jumatatu, 9 Mei 2016
Washtakiwa 21 wafungwa jela maisha Burundi
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
SOMA ZAIDI HAPA
-
Bonyeza hapa kuyaangalia moja kwa moja...
-
Image caption Magufuli: AirTanzania kupaa tena kufikia mwisho wa mwezi Septemba mwaka huu Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amet...
-
Magufuli apunguza kodi ya mapato na 2% Huku wafanyikazi kote duniani wakiadhimisha sikukuu ya wafanyakazi, nchini Tanzania, wafanyikazi wa...
-
Kundi moja la maafisa wa polisi limefanya maandamano karibu na tama...
-
WATU wawili wanaosadikika kuwa ni majambazi ambao wametokea Njombe wameuwawa katika majibizano ya risasi na polisi baada ya kuvamia Pub ya M...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza Kamishna wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernesti Mangu kumpandis...
-
Im Madaktari nchini India wamepandikiza pua mpya katika uso wa mvulana wa miaka 12 iliokuwa imemea katika paa lake la uso. Pua ...
-
Image caption Makamu wa rais Riek Machar Kushoto na Salva Kiir Kulia Taarifa kutoka Sudan Kusini zinasema mamia ya watu, wengi wa...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni