Maandamano yalianza Burundi Aprili mwaka jana
Mahakama ya rufaa nchini Burundi imewahukumu washtakiwa 21 vifungo vya maisha jela baada ya kuwapata na hatia ya kushiriki jaribio la mapinduzi mwaka jana.
Washtakiwa hao ni kati ya 28 waliokuwa wameshtakiwa kuhusiana na jaribio hilo la Mei mwaka jana ambalo halikufaulu.
Miongoni mwao ni watano ambao walikuwa wamepatikana bila hatia na mahakama ya kwanza.
Mahakama hiyo ya rufaa imeagiza wakamatwe.
Upande wa mashtaka ulikata rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa na mahakama ya chini ukisema hukumu hiyo haikuwa kali vya kutosha.
UN: Watu 474 wameuawa Burundi
Mataifa ya Kifaransa yavunja uhusiano wao na Burundi
Wale waliopatikana na hatia pia wametakiwa kulipa zaidi ya $3.5m (£2.4m) kama fidia kutokana na vifo na uharibifu wa mali uliotokea wakati wa jaribio hilo la kupindua serikali.
Baadhi ya majenerali kwenye jeshi na baadi ya maafisa wakuu katika idara ya polisi walijaribu kumpindua Rais Pierre Nkurunziza baada yake kuamua kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi wa leo unatazamwa kama ushindi wa serikali ambayo imekuwa ikijaribu kujenga uhusiano wa moja kwa moja baina ya jaribio hilo la mapinduzi na maandamano ya kupinga hatua ya Rais Nkurunziza kuwania kwa muhula wa tatu.
Maandamano hayo yalianza wiki mbili kabla ya mapinduzi.
BREAKING NEWS
-
Image copyright GETTY Image caption Michy alifunga dhidi ya Hungary baada ya kuingia nafasi ya Romelu Lukaku Klabu ya Chelsea ya Uingerez...
Jumatatu, 9 Mei 2016
Washtakiwa 21 wafungwa jela maisha Burundi
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
SOMA ZAIDI HAPA
-
Image copyright GETTY Image caption Michy alifunga dhidi ya Hungary baada ya kuingia nafasi ya Romelu Lukaku Klabu ya Chelsea ya Uingerez...
-
Image copyright REUTERS Polisi nchini Ufaransa wamewakamata watu watatu wanaohusishwa na shambulizi la lori la siku ya Alhamis mjini Nic...
-
Image copyright EPA Image caption Ethiopia imezima mitandao ya kijamii Mitandao ya kijamii nchini Ethiopia imezimwa. Waethiopia...
-
Kundi moja la maafisa wa polisi limefanya maandamano karibu na tama...
-
Wanasayansi wanadai kuunda aina ya ngozi inayoweza kubandikwa juu ya mwi...
-
Image copyright AP Image caption Waziri mmoja amesema watu hao walikuwa kwenye kundi la Mujahdeen Bangladesh wala sio Islamic State. Maa...
-
Kilimo cha miti kimepata umaarufu wa ghafla miaka ya hivi karibuni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ongezeko la mahitaji ya mazao ya m...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni