Maandamano yalianza Burundi Aprili mwaka jana
Mahakama ya rufaa nchini Burundi imewahukumu washtakiwa 21 vifungo vya maisha jela baada ya kuwapata na hatia ya kushiriki jaribio la mapinduzi mwaka jana.
Washtakiwa hao ni kati ya 28 waliokuwa wameshtakiwa kuhusiana na jaribio hilo la Mei mwaka jana ambalo halikufaulu.
Miongoni mwao ni watano ambao walikuwa wamepatikana bila hatia na mahakama ya kwanza.
Mahakama hiyo ya rufaa imeagiza wakamatwe.
Upande wa mashtaka ulikata rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa na mahakama ya chini ukisema hukumu hiyo haikuwa kali vya kutosha.
UN: Watu 474 wameuawa Burundi
Mataifa ya Kifaransa yavunja uhusiano wao na Burundi
Wale waliopatikana na hatia pia wametakiwa kulipa zaidi ya $3.5m (£2.4m) kama fidia kutokana na vifo na uharibifu wa mali uliotokea wakati wa jaribio hilo la kupindua serikali.
Baadhi ya majenerali kwenye jeshi na baadi ya maafisa wakuu katika idara ya polisi walijaribu kumpindua Rais Pierre Nkurunziza baada yake kuamua kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi wa leo unatazamwa kama ushindi wa serikali ambayo imekuwa ikijaribu kujenga uhusiano wa moja kwa moja baina ya jaribio hilo la mapinduzi na maandamano ya kupinga hatua ya Rais Nkurunziza kuwania kwa muhula wa tatu.
Maandamano hayo yalianza wiki mbili kabla ya mapinduzi.
BREAKING NEWS
-
Nucleated rural settlement Advantages More interaction with people. Safer as there are more people. Can share ideas on how to solve a p...
Jumatatu, 9 Mei 2016
Washtakiwa 21 wafungwa jela maisha Burundi
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
SOMA ZAIDI HAPA
-
Nucleated rural settlement Advantages More interaction with people. Safer as there are more people. Can share ideas on how to solve a p...
-
Image caption Taban Deng Gai Maafisa wa serikali ya Sudan Kusini wameiambia BBC kwamba wanamtambua waziri wa madini Taban Deng Gai kuwa ...
-
Im Madaktari nchini India wamepandikiza pua mpya katika uso wa mvulana wa miaka 12 iliokuwa imemea katika paa lake la uso. Pua ...
-
Image caption Mosul Iraq Viongozi wawili wakuu wa kundi la kigaidi la Islamic State waliuawa katika mashambulizi ya angani...
-
Image caption Makamu wa rais Riek Machar Kushoto na Salva Kiir Kulia Taarifa kutoka Sudan Kusini zinasema mamia ya watu, wengi wa...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni