Maandamano yalianza Burundi Aprili mwaka jana
Mahakama ya rufaa nchini Burundi imewahukumu washtakiwa 21 vifungo vya maisha jela baada ya kuwapata na hatia ya kushiriki jaribio la mapinduzi mwaka jana.
Washtakiwa hao ni kati ya 28 waliokuwa wameshtakiwa kuhusiana na jaribio hilo la Mei mwaka jana ambalo halikufaulu.
Miongoni mwao ni watano ambao walikuwa wamepatikana bila hatia na mahakama ya kwanza.
Mahakama hiyo ya rufaa imeagiza wakamatwe.
Upande wa mashtaka ulikata rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa na mahakama ya chini ukisema hukumu hiyo haikuwa kali vya kutosha.
UN: Watu 474 wameuawa Burundi
Mataifa ya Kifaransa yavunja uhusiano wao na Burundi
Wale waliopatikana na hatia pia wametakiwa kulipa zaidi ya $3.5m (£2.4m) kama fidia kutokana na vifo na uharibifu wa mali uliotokea wakati wa jaribio hilo la kupindua serikali.
Baadhi ya majenerali kwenye jeshi na baadi ya maafisa wakuu katika idara ya polisi walijaribu kumpindua Rais Pierre Nkurunziza baada yake kuamua kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi wa leo unatazamwa kama ushindi wa serikali ambayo imekuwa ikijaribu kujenga uhusiano wa moja kwa moja baina ya jaribio hilo la mapinduzi na maandamano ya kupinga hatua ya Rais Nkurunziza kuwania kwa muhula wa tatu.
Maandamano hayo yalianza wiki mbili kabla ya mapinduzi.
BREAKING NEWS
-
Introduction What is a teaching portfolio? A teaching portfolio is a collection of documents tha...
-
Mwanamke ambaye anataka kutumia mayai ya uzazi ya bintinye ili kumzaa mjukuu wake ameshinda kesi mahakanani na kuruhusiwa kufanya...
Jumatatu, 9 Mei 2016
Washtakiwa 21 wafungwa jela maisha Burundi
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
SOMA ZAIDI HAPA
-
Introduction What is a teaching portfolio? A teaching portfolio is a collection of documents tha...
-
Mwanamke ambaye anataka kutumia mayai ya uzazi ya bintinye ili kumzaa mjukuu wake ameshinda kesi mahakanani na kuruhusiwa kufanya...
-
Mshirikishe mwenzako Image caption Kuondoa sheria hiyo ilikuwa moja ya vipaumbele vya Trump alipokuwa akiwania urais Makamu wa...
-
What is Sociolinguistics? One of the goals of the MLC is to equip students with a solid knowledge – both theoretical and practic...
-
Published Under SIASA Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema hataki kuwaona nyumbani kwake wasanii ambao wamekacha...
-
Mabingwa wa Ligi Kuu ya England Leicester City wamekubaliana na CSKA Moscow kumsajili mshambuliaji kutoka Nigeria Ahmed Musa. Hii ni kwa m...
-
Image caption Taban Deng Gai Maafisa wa serikali ya Sudan Kusini wameiambia BBC kwamba wanamtambua waziri wa madini Taban Deng Gai kuwa ...
-
Leo tarehe 3 julai Waziri Mkuu wa zamani Mh. Edward N Lowassa alikua moja wa wageni waalikwa sambamba na Rais wa Jamuhuri ya Kenya, Uhur...
-
N MKOA NAMBA YA SHULE JINA LA SHULE JINSI JINA 1 GEITA S1164 MISSUNGWI SECONDARY SCHOOL F ...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni