BREAKING NEWS

Jumamosi, 14 Mei 2016

Serena Williams ala chakula cha mbwa


Nyota wa mchezo wa tenisi kwa upande wa wanawake Serena Williams alijitia ugonjwa baada ya kula chakula cha mbwa saa chache kabla ya kufuzu katika robo fainali ya mashindano ya Italian Open.
Serena alijaribu kula kijiko kimoja cha chakula cha mbwa wake kabla ya kumshinda Mmarekani mwenzake Christina McHale katika seti za moja kwa moja.
''Nilisema kwani kuna nini,nitajaribu kipande kimoja,kinaonja utamu'',alisema.
''Lakini mda mchache nililazimika kukimbia chooni kama ambaye ningezimia''.
''Chakula kilikuwa na ladha mbaya''.
''Kinaonja kama dawa ya kusafisha nyumba''.Katika video ya Snap chat ,wiliams alielezea kuwa alichukua samaki na wali uliokuwa katika chakula kilichopewa mbwa katika hoteli aliyokuwa akilala.
''Nilijilazimisha kula'',alisema mchezaji huyo wa Marekani mwenye umri wa miaka 34.
''Sijui wanatia nini katika chakula hiki cha mbwa,lakini mbwa alikipenda sana

Mwanamume 'adandia' helikopta Bungoma Kenya

Ndege

Mwanamume mmoja katika mji wa Bungoma, Magharibi mwa Kenya ameshangaza wengi baada ya kudandia helikopta ambayo imepaa na kuondoka naye.
Helikopta hiyo ilikuwa imesafirisha mwili wa mfanyabiashara mashuhuri Jacob Juma aliyeuawa kwa kupigwa risasi jijini Nairobi wiki iliyopita, vyombo vya habari nchini Kenya vinasema.
Video zinazosambaa mtandaoni zinaonesha helikopta hiyo ikipaa juu angani kutoka uwanja wa Posta, mwanamume huyo akiwa amejishikilia kwenye vyuma vya helikopta hiyo.
Taarifa zinasema baadaye ndege imetua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Bungoma na mwanamume huyo akapelekwa hospitalini.

Paka mzee zaidi kutoka Marekani afariki


 
Paka aliyewekwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Guiness of World record kwa kuwa mzee amefariki.
Scooter aliyesheherekea miaka 30 ya kuzaliwa mnamo mwezi Machi amefariki.
Mmiliki wake Gail Floyd kutoka Texas amesema kuwa paka huyo alifariki baada ya kuthibitishwa kuwa mzee zaidi.
Daktari Tricia Latimer,amesema kuwa Scooter aliishi kwa karibia miaka 136 ya binaadamu na amekuwa akisafiri mara kwa mara.
Kufikia sasa alikuwa ametembea majimbo 45 kati ya 50 ya Marekani

Alhamisi, 12 Mei 2016

NAFASI 11 ZA KAZI KILIMANJARO AIRPORTS DEVELOPMENT COMPANY(KADCO) MWISHO WA KUTUMA MAOMBI NI TAREHE 23 MAY 2016





Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO) is a company owned by the Government of United Republic of Tanzania charged to manage and develop Kilimanjaro International Airport and its estate.

KADCO is seeking to employ competent, experienced, highly organized and self-motivated Tanzanias to fill the vacant positions described below:-

1. Procurement Officer
2. Assistant Stores Officer
3. Internal Auditor
4. Laboratory Technician
5. Pharmaceutical Technician
6. Company Secretary
7. Head of Planning and Statistics
8. Accounts Officers
9. Drivers
10. Firemen Commanding Officers
11. Nurse Officer II

General Conditions
-Interested and qualified Tanzanians advised to submit their application letter enclosed updated Curriculum Vitae (CV) bearing reliable contacts i.e postal address, e-mail address and reliable mobile phone numbers, certified photocopy of the original academic/Professional Certificates, one recent passport size picture, birth certificate to

Managing Director,
P.O. Box 10,
Kilimanjaro International Airport (KIA)
Tanzania

-Application letter, the envelop or subject line of the email should bear the Ref. No. of the post applied. Application without Ref. No. shall not be considered.
-Testimonials, Partial transcripts and results slip will not be accepted.
-Certificates from foreign Universities/ examination bodies should be verified by The Tanzania Commission for Universities (TCU) and National Examination Council of Tanzania (NECTA)
-Applications should indicate three reputable referees with their reliable contacts.
-Application letters should be written in english.
-Presenting of forged academic certificates and other incorrect information in CV shall amount to legal actions.
-Applicants with special needs/cases or disabilities are encouraged to apply and are supposed to indicate their physical status in their application letter.
-All applicants must be submitted not later than 23rd May, 2016 at 1530 local time.

KADCO is an equal opportunity employer: Only qualified candidates will be contacted

Source: Mwananchi 11th May, 2016

Polisi waandamana dhidi ya Beyonce




Kundi moja la maafisa wa polisi limefanya maandamano karibu na tamasha lililofanyika katika mji wa nyumbani wa nyota wa muziki Beyonce huko Houston.
Wanachama wa muungano wa polisi na Sherrif walisimama mbali na uwanja wa soka na kuelekeza mwangaza wa bluu katika ukumbi wa tamasha hilo.
Walikuwa wanapinga kanda ya video ya Beyonce ambayo wanasema inawaponza polisi.
 

Mwanamuziki huyo tayari amesema kwamba hawakosoi polisi katika wimbo huo na kusema kuwa maafisa wa polisi wanaodhani aliwaponza wanakosea.
Mwanachama mmoja wa polisi amekiambia chombo cha habari KHOU11 kwamba hawakufurahia baada ya Beyonce kutumia picha za gari moja la polisi mjini New Orleans iliokuwa ikizama katikamafuriko.
''Tunaamini kwamba baadhi ya mambo yake ni kinyume na maafisa wa polisi'',alisema.

Mnamo mwezi Aprili,Beyonce aliambia jarida la Elle kwamba anaheshimu polisi lakini hapendi unyanyasaji.
''Mtu yoyote anyedhani kwamba siwapendi polisi anakosa kwa sababu'', alisema.
''Ninawapenda na kuwaheshimu sana polisi pamoja na familia za maafisa hao ambao hujitolea ili kuhakikisha tuko salama''.

Walimu walipwa vifaranga badala ya mshahara Uzbekistan

walimuwalipwa kuku badala ya mishahara

Mji mmoja nchini Uzbekistan umekua ukiwapa waalimu wake kuku kama mshahara badala ya pesa. Mamlaka za mji wa Nukus katika jimbo linalojitawala la Karakalpakstan wamekua wakitia vifaranga wachanga kwa walimu kutokana na uhaba wa pesa nchini humo.
Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Marekani{Radio Ozodlik} kimemnukuu mwalimu mmoja akilaani hatua hiyo kama aibu kubwa kwa mamlaka.
Mwalimu huyo aliyeghadhabishwa na hatua hiyo amesema hataki vifaranga kwa sababu anaweza kuwapata sokoni, lakini wanataka pesa zao.
Vifaranga wanaotolewa kama mshahara wana gharama ya dola mbili kila mmoja, ikiwa ni maradufu bei inayouzwa vifaranga sokoni.
Mamlaka za Uzbekistan hazikubalii uhuru wa vyombo vya habari na raia wa huko hutegemea vyombo vya habari vya kimataifa kutoa sauti yao, ila hawajitambulishi.
Uzbekistan imekumbwa na uhaba wa fedha kwa miaka sasa hali inayosababisha serikali kuchelewesha mishahara ya wafanyikazi na malipo ya uzeeni.
Mapema mwezi huu wafanyikazi wa serikali katika mji mkuu,Tashkent walilalamikia kwamba hawakuwa wamelipwa mshahara kwa miezi miwili kwa sababu benki hazikuwa na pesa.

Mwanamke wa miaka 72 ajifungua mtoto India

Daljinder Kaur

Mwanamke wa umri wa miaka 72 amejifungua mtoto mvulana katika hospitali moja nchini India.
Mwanamke huyo alipachikwa mimba kupitia njia ya kitaalamu ya IVF ambapo yai la mwanamke hutolewa kutoka kwenye ovari, kutungishwa mbegu ya kiume na kisha kurejeshwa kwenye mji wa mimba. Yai hilo linaweza kutolewa kwa mwanamke mwingine.
Njia hiyo hutumiwa kuwawezesha wanawake tasa kupata watoto.
Daljinder Kaur alijifungua mtoto wake baada ya kupokea matibabu kwa miaka miwili katika hospitali iliyoko jimbo la Haryana.
Matabibu walifanikiwa kumtungisha mimba kupitia IVF mara yao ya tatu.
Mumewe Kaur ana umri wa miaka 79.
Kisa hicho kimezua mjadala mkali kuhusu kutumiwa kwa teknolojia hiyo ya IVF na umri ambao wanawake wanaweza kuruhusiwa kuitumia kupata watoto.
Dkt Kanad Nayar, katibu mkuu wa chama cha upachikaji mimba nchini India anasema sheria ya kuamua umri wa juu ambao mwanamke anaweza kuruhusiwa kutumia teknolojia hiyo itatungwa karibuni.
Sana umri huo utakuwa miaka karibu miaka 55.
Daktari huyo anasema jambo la kuzingatiwa zaidi ni uwezo wa mwanamke kumlea mtoto hadi akomae.

Wanasayansi waunda ngozi kuziba uzee



Wanasayansi wanadai kuunda aina ya ngozi inayoweza kubandikwa juu ya mwili wa mtu kupunguza muonekano wa mikunjo ya ngozi mwilini na ngozi inayopwaya chini ya macho kutokana na uzee.Ni aina ya maji maji mtu anayopaka mwilini alafu inaachwa kukauka ambapo baadaye husihia kuwa ngozi nyembamba iliyo mithili ya 'ngozi ya ujana, Nature Materials inaarifu baada ya kufanya majiribio kadhaa madogo.
Kwa sasa inafanyiwa majaribio ya kuuzwa kama bidhaa ya urembo.
Lakini wanasayansi Marekani wanasema "ngozi ya pili " huenda baadaye ikaweza kutumika kutengeneza dawa na kinga dhdi ya jua.
Ngozi ya piliKundi la wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Havard kitengo cha matibabu na taasisi ya teknolojia Massachusetts wamefanya majaribio ya bidhaa hiyo kwa watu waliojitolea ambao walipakwa ngozi hiyo chini ya macho, kwenye mikoni yao na miguu.
Ngozi hiyo inayotokana na kemikali polysiloxane polymer iliundwa kwenye maabara kwa kutumia chembe chembe za Silicone na hewa safi ya Oxygen.
Licha ya kwamba sio ngozi ya kweli lakini imeundwa kuiga ngozi asili na pia kuacha nafasi ya hewa kupita.
Kwa mujibu wa watatfiti ngozi hiyo bandia ina uwezo wa kunasa mvuke na kusaidia ngozi kujivuta kiasi cha inavyostahili.

Rais wa Brazil Dilma Rousseff asimamishwa kazi

 
Bunge la Seneti Brazil limepiga kura kuamua kuidhinisha kura ya kutokuwa na imani dhidi ya kiongozi wa taifa hilo Dilma Rousseff.
Atasimamishwa kazi ya urais kwa siku zisizozidi 180 wakati bunge hilo la Seneti litakagua tuhuma zinazomkabili.
Bi Rousseff anatuhumiwa kubadili kinyume cha sheria fedha za serikali kuficha nakisi inayoongezeka ya umma kufuatia kuchaguliwa kwake tena mnamo 2014, tuhuma anazozikana.
Masenata 55 waliunga kuidhinishwa kura hiyo ya kutokuwana imani dhidi ya 22 bungeni katika kikao cha zaidi ya saa 20.
Makamu wa rais Michel Temer sasa ndio atashikilia madaraka wakati kesi dhidi ya Bi Rousseff inaendelea.
Rousseff alichukua hatua ya mwisho kujiokoa kwa kukataa rufaa katika mahakama ya juu zaidi nchini humo kusitisha kura hiyo, lakini hatua hiyo ilipingwa.

KINYAMBE AFARIKI DUNIA

TANZIA: Mwigizaji wa comedy Mohammed Abdallah maarufu "Kinyambe" amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya mkoa wa Mbeya alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Mungu amlaze mahali pema peponi ndugu yetu Kinyambi. #RIP

Jumatatu, 9 Mei 2016

GE 349: SEMINAR QUESTION

Examine why Africa's mineral and energy resources have not stimulated real economic development in the content.

Washtakiwa 21 wafungwa jela maisha Burundi

Maandamano yalianza Burundi Aprili mwaka jana
Mahakama ya rufaa nchini Burundi imewahukumu washtakiwa 21 vifungo vya maisha jela baada ya kuwapata na hatia ya kushiriki jaribio la mapinduzi mwaka jana.
Washtakiwa hao ni kati ya 28 waliokuwa wameshtakiwa kuhusiana na jaribio hilo la Mei mwaka jana ambalo halikufaulu.
Miongoni mwao ni watano ambao walikuwa wamepatikana bila hatia na mahakama ya kwanza.
Mahakama hiyo ya rufaa imeagiza wakamatwe.
Upande wa mashtaka ulikata rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa na mahakama ya chini ukisema hukumu hiyo haikuwa kali vya kutosha.
UN: Watu 474 wameuawa Burundi
Mataifa ya Kifaransa yavunja uhusiano wao na Burundi
Wale waliopatikana na hatia pia wametakiwa kulipa zaidi ya $3.5m (£2.4m) kama fidia kutokana na vifo na uharibifu wa mali uliotokea wakati wa jaribio hilo la kupindua serikali.
Baadhi ya majenerali kwenye jeshi na baadi ya maafisa wakuu katika idara ya polisi walijaribu kumpindua Rais Pierre Nkurunziza baada yake kuamua kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi wa leo unatazamwa kama ushindi wa serikali ambayo imekuwa ikijaribu kujenga uhusiano wa moja kwa moja baina ya jaribio hilo la mapinduzi na maandamano ya kupinga hatua ya Rais Nkurunziza kuwania kwa muhula wa tatu.
Maandamano hayo yalianza wiki mbili kabla ya mapinduzi.

SOMA ZAIDI HAPA