BREAKING NEWS

Jumamosi, 16 Julai 2016

Wanajeshi waasi 104 wauawa Uturuki



Image copyrightGETTY
Naibu mkuu wa jeshi la Uturuki ametangaza kwa njia ya runinga kuwa jaribio la mapinduzi ya kijeshi limeshindwa.
Jenerali Umit Dundar alisema kuwa wapanga mapinduzi 104 wameuauwa. Pia amesema kuwa watu wengine 90 wakiwemo polisi na raia wameuawa.
Usiku kucha miji ya Ankara na Istanbul ilikumbwa na milio ya risasi na milipuko baada ya wanajeshi waasi kufanya mashambulizi wakitumia vifaru na helikopta.
Maafisa wanasema kuwa zaidi ya wanajeshi 1500 wamekamatwa huku wale wa vyeo vya juu wakiwemo majerali wakipokonywa nyadhifa zao.

Unyonyaji kidole unafaida kwa watoto- Utafiti


Image copyrightTHINKSTOCK
Image captionUnyonyaji kidole unafaida kwa watoto- Utafiti
Ripoti mpya inasema watoto wanaonyonya vidole au kung'ata kucha zao kwa meno huenda wasipate matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani.
Kwa mujibu wa waandishi katika jarida la Pediatrics, huo ni ni usafi dhanio,kwani yatokanayo na baadhi ya wadudu huimarisha mfumo wa kinga ya mwili.
Unyonyaji wa kidole gumba na ung’ataji wa kucha umeonekana kuzuia baadhi ya alergy.
Kati ya watu elfu moja wenye umri wa kati ya miaka mitano hadi thelathini na mbili,walifanyiwa uchunguzi kwa muda nchini New Zealand.
Lakini tabia hii ya unyonyaji vidole na ung’ataji kucha haisaidii watu wenye pumu au mtu anapopata homa kali.
Uchunguzi uliofanywa na kurekodiwa kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka mitano na kumi na moja na wengine waliofanyiwa vipimo ni wenye umri kati ya miaka kumi na tatu na thelathini na miwili.
Huku thuluthi moja ya watoto hao ni wanyonyaji wa vidole mara kwa mara au hung’ata kucha zao na katika vipimo walivyofanyiwa watoto hao wameonekana kuwa wana kiwango kidogo cha kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani.
Image copyrightTHINKSTOCK
Image captionLakini tabia hii ya unyonyaji vidole na ung’ataji kucha haisaidii watu wenye pumu au mtu anapopata homa kali.
Watoto wanaoweza kupata matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani (alergy) kutokana na vitu kama vumbi kutoka majumbani,manyoya ya paka au mbwa, lakini watoto wenye kunyonya vidole gumba na kung’ata kucha walikuwa ni chini ya theluthi moja kuliko watoto wenye tabia hii ya unyonywaji vidole.
Na tabia hii ya unyonyaji vidole au ung’ataji kucha inaonekana kuwa kinga mpaka wanapofikia umri wa utu uzima.
" kuwa na paka au mbwa majumbani,ndugu au jamaa wanaofanya kazi mashambani pia imeonekana kuwa ni sababu kubwa inayosababisha mazingira ya ukuaji wa magonjwa yanayosababishwa na
kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani

Mamia wapigwa picha wakiwa utupu Uingereza


Alfred GelderImage copyrightAFP
Image captionBarabara ya Alfred Gelder iligeuzwa kuwa bahari ya watu
Watu zaidi ya 3,000 walipigwa picha wakiwa utupu nchini Uingereza chini ya mradi wa kuadhimisha na kusherehekea utamaduni.
Mradi huo uliopewa jina Bahari ya Hull unatumiwa kusherehekea mji wa Hull kama Mji wa Utamaduni kwenye sherehe kuu mwaka ujao.
Baraza la Jiji la Hull lilisema mradi huo wa sanaa, ndio mkubwa zaidi wa aina yake kufanyika Uingereza.
Image copyrightAFP
Uliendeshwa na mpigapicha mashuhuri duniani Spencer Tunick na kushirikisha watu 3,200 kutoka nchi 20, ambao walipigwa picha katika maeneo mbalimbali maarufu mjini humo Jumamosi iliyopita.
WalioshirikiImage copyrightREUTERS
Image captionWatu wa kujitolea kutoka nchi 20 walishiriki
Picha hizo, ambazo zinasimamiwa na shirika la maonesho ya Sanaa la Ferens Art Gallery, zitawekwa kwenye maonesho wakati wa shughuli za Jiji la Utamaduni Uingereza mwaka 2017.
Maelfu ya watu walifika kabla ya jua kuchomoza na wakapakwa rangi ya samawati iliyokozwa kwa viwango vinne, kuashiria maji.

Walipigiwa picha maeneo mbalimbali yakiwemo Bustani ya Malkia, Guildhall na daraja la Scale Lane.
Shughuli yote ilidumu saa nne.
Image copyrightAP
Mmoja wa walioshiriki alikuwa Stephane Janssen, mwenye umri wa miaka 80 anayetoka Brussels.
Ameshiriki miradi ya upigaji picha wa watu wengi wakiwa utupu ya Tunick mara 20 awali.
TunickImage copyrightPA
Image captionBw Tunick (kushoto) akiwa na Janssen
“Ni maridadi sana, ni kupakwa rangi kidogo tu. Kila mtu ni sawa – hakuna tofauti ya rangi au jinsia – kila mtu ni sawa na yule mwingine akiwa utupu, na hilo ndilo napenda,” alisema.
Sarah Hossack, kutoka Hull, alisema alifurahia sana.
Image copyrightAFP
“Nilikuwa utupu tangu saa kumi alfajiri. Lakini nilifurahia sana. Shughuli hiyo ilituleta pamoja,” alisema.
Mradi huo wa Hull uliushinda ule wa Gateshead wa mwaka 2005 ambapo ni watu 1,700 waliojitokeza pamoja na ule wa Salford wa mwaka 2010 ambapo watu 1,000 walishiriki.
Image copyrightAFP
Kirsten Simister, afisa katika Ferens Art Gallery, alisema alishangazwa sana na idadi ya watu waliojitokeza Hull.
Tunick, ambaye makao yake ni New York, amefanya miradi mingine 90 kama huo wa Hull.
Amewahi kupigia watu wengi kwa pamoja picha katika Sydney Opera House, Place des Arts mjini Montreal, Mexico City na Munich nchini Ujerumani.

Bikizee wa miaka 94 arejea kazini Marekani


SoskinImage copyrightAP
Image captionBi Soskin (kati) alipokelewa kwa furaha kuu na wafanyakazi wenzake
Mama mmoja Mmarekani mwenye umri wa miaka 94 amerudi kazini kama askari waitwao Park Pangers wa kuhuduma katika mbuga na hifadhi za kitaifa nchini Marekani.
Bi Betty Reid Soskin, alikuwa ameacha kazi baada ya mkasa kumkumba ulimfanya.
Katika mkasa huo mwizi alimvamia nyumbani kwake tarehe 27 Juni, akamgonga ngumi kichwani na kumwibia simu, tarakilishi, vito vya thamani na hata medali yake aliyokuwa ametunukiwa na rais Obama.
Lakini anasema alitaka sana kurejelea maisha aliyoyazoea.
Bi Soskin, alikuwa mwelekezi katika hifadhi ya kihistoria iliyoko eneo la San Francisco Bay kwa muda wa miaka 10.
Kama anavyoonekana katika picha hizo za makaribisho ya wafanyikazi wenzake hapo hifadhi ya Rosie the Riveter World War Two Home Front National Historical Park ni vigumu kukadiria umri wakeread more.

Wafungwa 3 wauwa gerezani Thailand




Image copyrightEPA
Wafungwa watatu wameuawa wakati wa maandamano kwenye gereza moja lililo kusini mwa Thailand.
Karibu wafungwa 100 walishiriki katika ghasia hizo kwenye gereza moja lililo mkoa wa Pattani, ambazo zilidumu kwa muda wa saa sita.
Wafungwa hao kwanza walichoma majengo mawili ndani ya gereza hilo.
Wafungwa hao walikuwa wametangaza matakwa kadha ikiwemo kutembelewa zaidi na familia zao na pia kupewa fursa ya kutizama habari kwenye runinga.

Washukiwa 3 wa shambulizi wakamatwa Ufaransa


Image copyrightREUTERS
Polisi nchini Ufaransa wamewakamata watu watatu wanaohusishwa na shambulizi la lori la siku ya Alhamis mjini Nice lililosababisha vifo vya watu 84.
Wale waliouawa walikuwa kati ya umati mkubwa uliokuwa ukitizama maonyesho ya fataki, wakati lori lilivurumishwa makusudi kwenda eneo walikuwa.
Zaidi ya watu 50 wako hali mahututi hospitalini. Siku tatu za maombolezi zimeanza kwa waathiriwa wanaotoka nchi kadha.

Nyimbo kumi bora zaidi kwa harusi duniani


EdImage copyrightGETTY
Image captionEd Sheeran, 25, akiwa na mashabiki
Wimbo wa mapenzi wa mwanamuziki wa Uingereza Ed Sheeran unaongoza kwa kupendwa sana na watu kama wimbo wa kufungua jukwaa wakati wa harusi.
Kwa mujibu wa mtandao wa Spotify, ambao wamechunguza maelfu ya orodha ya nyimbo zinazosambazwa zaidi katika mtandao huo, wimbo wa Thinking Out Loud unaongoza.
Wimbo wa At Last wake Etta James ni wa pili nao wimbo wa Ray LaMontagne, You Are the Best Thing ni wa tatu.
Nyimbo nyingine maarufu zilizo kwenye orodha ya 50 bora duniani ni wimbo wake Frank Sinatra uitwao The Way You Look Tonight na wimbo wa Marry You wake Bruno Mars.
SheeranImage copyrightGETTY
Image captionJina halisi la Sheeran ni Edward Christopher "Ed" Sheeran
Nyimbo kumi zinazopendwa zaidi duniani kwa mujibu wa Spotify, mtandao unaowawezesha watu kusikiliza nyimbo moja kwa moja mtandaoni, ni:
  1. Thinking Out Loud - Ed Sheeran
  2. At Last - Etta James
  3. You Are the Best Thing - Ray LaMontagne
  4. All of Me - John Legend
  5. A Thousand Years - Christina Perri
  6. Make You Feel My Love - Adele
  7. I Won’t Give Up - Jason Mraz
  8. Everything - Michael Bublé
  9. Better Together - Jack Johnson
  10. Amazed - Lonesta

SHULE 10 BORA KWENYE MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2016

Shule 10 zilizofanya vizuri:

1.Kisimiri,-Arusha
2.Feza Boys,-Dar es Salaam
3.Alliance Girls,-Mwanza
4. Feza Girls,-Dar es Salaam
5. Marian Boys,-Pwani
6.Tabora Boys,-Tabora
7.Kibaha,-Pwani
8.Mzumbe-Morogoro
9.Ilboru,-Arusha
10.Tandahimba-Mtwara

Shule 10 zilizofanya vibaya:

1.Mpendae-Unguja
2.Ben Bella-Unguja
3.Tumekuja-Unguja
4.Green Bird Boys-Kilimanjaro
5.Jang'ombe-Unguja
6.Kiembe Samaki-Unguja
7.Tanzania Adventist-Arusha
8.Al- Ishan Girls-Unguja
9.Azania-Dar es Salaam
10.Lumumba-Unguja

Ijumaa, 15 Julai 2016

Wapinzani wa Yanga Medeama watua Dar


YangaImage copyrightTFF TWITTER
Image captionYanga watakutana na Medeama Jumamosi saa kumi jioni
Wapinzani wa klabu ya Young Africans, katika michuano ya kuwania Kombe la Shirikisho Barani Afrika, Medeama kutoka Ghana, wametua Dar es Salaam tayari kwa mechi baina ya timu hizo Jumamosi.
Wachezaji hao waliwasili Dar Alhamisi na wakafanya mazoezi katika uwanja wa Karume.
Yanga itaikaribisha Medeama kwa mchezo wa tatu kuwania taji hilo hatua ya makundi katika uwanja wa taifa Dar es Salaam.
Mchezao huo utaanza saa 10.00 jioni
Michezo miwili ya awali ya Yanga katika michuano hiyo ilikuwa ni dhidi ya Mo Bejaia ya Algeria ambako ilipoteza kwa bao 1-0 kabla ya kupoteza tena dhidi ya TP Mazembe, mechi iliyopigwa jijini Dar es Salaam.
Mchezo wa Jumamosi utachezeshwa na waamuzi kutoka Misri ambao ni Ibrahim Nour El Din atakayekuwa mwamuzi wa kati; akisaidiwa na Ayman Degaish na Samir Gamal Saad wakati mwamuzi wa akiba akiwa ni Mohamed Maarouf Eid Mansour, kwa mujibu wa Shirikisho la Kandanda la Tanzania (TFF)

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA ( ACSEE) 2016 EXAMINATION RESULTS

BONYEZA HAPA KUANGALIA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA  2016

Jumatatu, 11 Julai 2016

Daktari feki akamatwa katika chumba cha wagonjwa mahututi hospitali ya Rufaa Morogoro


SeeBait
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Zakaria Benjamini mkazi wa Tungi Manispaa ya Morogoro baada ya kuingia hospitali ya rufaa kwa nia ya kufanya utapeli na kutaka kutoa huduma kwa wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi hilo Ulrich Matei amesema mtu huyo ameshikiliwa na jeshi hilo kufuatia tuhuma zinazo mkabili na mara baada ya kubaini ukweli wa jambo hilo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.

Daktari feki akamatwa katika chumba cha wagonjwa mahututi hospitali ya Rufaa Morogoro


SeeBait
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Zakaria Benjamini mkazi wa Tungi Manispaa ya Morogoro baada ya kuingia hospitali ya rufaa kwa nia ya kufanya utapeli na kutaka kutoa huduma kwa wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi hilo Ulrich Matei amesema mtu huyo ameshikiliwa na jeshi hilo kufuatia tuhuma zinazo mkabili na mara baada ya kubaini ukweli wa jambo hilo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.

Mchezaji wa ureno aliyefunga bao la ushidi

Kwa Picha: Mchezaji Eder wa Ureno aliyefunga bao la ushindi Euro 2016 dhidi ya Ufaransa. Jina lake kamili ni Éderzito António Macedo Lopes

Mashabiki Ureno waendelea kusherehekea


Image copyrightAFP
Image captionHii ni mara ya kwanza kwa Ureno kushinda taji kubwa kama hilo.
Kundi kubwa la mashabiki wa Ureno limeendelea kusheherekea bada ya timu yao ya taifa kuifunga Ufaransa katika michuano ya Euro 2016 mjini Paris.
Ureno imeshinda 1-0 katika muda wa nyongeza na kuwaacha mashabiki wa Ufaransa katika hali ya simanzi ndani ya dimba la Stade de France huku mitaa ya Lisbon ikirindima kwa shangwe kubwa.
Ureno illicheka karibia mda wote bila huduma ya nyota wake Cristiano Ronaldo aliyeumia na kutolewa nje dakika 25 ya mchezo huo na baadaye kurejea na kulinyanyua kombe hilo.
Amesema kombe hilo ni kwa ajili ya Wareno wote pamoja na wote wanaioshabikia timu hiyo mjini Paris.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ureno kushinda taji kubwa kama hilo.

SOMA ZAIDI HAPA