Jumatatu, 11 Julai 2016

Daktari feki akamatwa katika chumba cha wagonjwa mahututi hospitali ya Rufaa Morogoro


SeeBait
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Zakaria Benjamini mkazi wa Tungi Manispaa ya Morogoro baada ya kuingia hospitali ya rufaa kwa nia ya kufanya utapeli na kutaka kutoa huduma kwa wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi hilo Ulrich Matei amesema mtu huyo ameshikiliwa na jeshi hilo kufuatia tuhuma zinazo mkabili na mara baada ya kubaini ukweli wa jambo hilo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

SOMA ZAIDI HAPA