Jumamosi, 9 Julai 2016

Al-Shabab wavamia kituo cha polisi Kenya


Image copyrightAP
Image captionAl_shabab_kenya
Polisi nchini Kenya wanasema kuwa zaidi ya wapiganaji 100 wamevamia kituo kimoja cha polisi kaskazini mashariki mwa Kenya.
Wanasema wapiganaji wa al-Shabab waliingia mji wa Wajir wakiwa katika malori matatu saa za alfajiri siku ya Jumamosi.
Walirusha makombora ya roketi kabla ya kuondoka na silaha na magwanda ya polisi.
Image copyrightAFP
Image captionAlshabab
Polisi mmoja alijeruhiwa.Wapiganaji wa al-Shabab hutekeleza uvamizi wa mara kwa mara nchini Kenya ,mara nyengine wakivuka mpaka kutoka Somalia.
Kundi hilo pi lina wanachama wake wanaoishi nchini Kenya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

SOMA ZAIDI HAPA