BREAKING NEWS

Ijumaa, 6 Mei 2016

Walimu wagoma, kisa mwenzao kuzabwa kofi darasani


������������

WALIMU wa shule ya msingi Kianda wameanza mgomo wa siku mbili wa kutofundisha shuleni hapo huku wakilaani kitendo cha Ofisa Elimu (Shule za Msingi) wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Peter Fusi kumshambulia na kumpiga makofi mwalimu mwenzao akiwa darasani mbele ya wanafunzi wake.

Makamu Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Flora Kipesha alisema wameitisha mgomo huo wa siku mbili kupinga kitendo cha Fusi kumshambulia na kumpiga makofi mwalimu mwenzao Jacob Msengezi (25) ambaye anafundisha somo la Hisabati Darasa la Saba shuleni hapo.

“Licha ya kulaani vikali kitendo hiki cha udhalilishaji alichofanyiwa mwalimu mwenzetu na Ofisa Elimu (DEO) wetu (Peter Fusi) kumcharaza makofi mbele ya wanafunzi wake akiwa darasani ….

Ametudhalilisha sote yaani hata hamasa ya kufundisha imetoweka ….. “Sasa hatutaingia darasani kufundisha kwa siku mbili tukimshinikiza Mkurugenzi wa Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga (Adam Missana) achukue hatua dhidi ya ofisa huyo wa elimu ……yaani tunadhalilishwa hivi mbele ya wanafunzi wetu wenyewe wakati kazi hii tumeisomea na tuna vyeti halali ….

Tukiwa na sifa stahiki za taaluma ya ualimu,” alieleza Kipesha. Akifafanua, alisema walimu hawataingia kufundisha kwa siku hizo mbili na watakuwa ofisini wakiandaa mitihani huku wanafunzi wakiendelea kuhudhuria shuleni hapo kama kawaida.

Naye Mwalimu Msengezi alilieleza gazeti hili kwa njia ya simu akiwa shuleni Kianda kuwa juzi Jumatano Ofisa Elimu, Fusi alitembelea shuleni hapo saa tatu asubuhi akikagua mazingira ya shule.

“Mie wakati huo nilikuwa darasani na wanafunzi wa darasa la saba nikisahihisha madaftari yao kwani tayari kipindi changu kilianza saa 2:00 na kumalizika 2:40 asubuhi … Hivyo kwa kuwa mwalimu wa somo la Kiingereza alikuwa ‘busy’ akitunga mitihani niliamua niutumie muda huo kubaki darasani humo nikisahihisha madaftari,” alieleza Msengezi Kwa upande wake, Katibu wa CWT Wilaya ya Sumbawanga Vijijini, Vicent Ndewele akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu alikiri kutokea kwa tukio hilo huku akisisitiza kuwa chama hicho kitatoa msimamo wake leo.☝☝☝☝☝☝☝Hawa Maafisa Huwa wanakutana Na,Walimu Wapole Tu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

SOMA ZAIDI HAPA